2013-05-08 09:36:21

Kardinali Pengo: simameni kidete kusema na kutetea ukweli ili kujenga amani!


Mama Kanisa anapoendelea kuadhimisha Jubilee ya Miaka 50 tangu Baba Mtakatifu Yohane wa Ishirini na tatu alipochapisha Waraka "Pacem in Terris" "Amani Duniani" anakumbusha kwamba, amani kimsingi inasimikwa katika mihimili mikuu minne: Yaani: Ukweli, haki, uhuru na upendo unaojionesha katika mshikamano wa dhati baina ya watu ndani ya Jamii.

Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam, akirejea kuhusu tukio la kigaidi lililotokea Jimbo kuu la Arusha, Jumapili tarehe 5 Mei 2013 na kusababisha maafa makubwa anasema, amani ya kweli nchini Tanzania itajengwa katika msingi wa ukweli bila kuupotosha wala kuupindisha. Watu wajifunze kusimama kidete kusema na kutetea ukweli!

Kardinali Pengo anakazia kwamba, amani ya Tanzania ni jambo la msingi linalopaswa kupewa kipaumbele cha kwanza. Kujaribu kuficha au kupotosha ukweli ni kutaka kumfungulia njia Ibilisi ili aweze kuleta vurugu na kinzani miongoni mwa Watanzania.







All the contents on this site are copyrighted ©.