Askofu mkuu Josephat Lebulu wa Jimbo kuu la Arusha Tanzania, mara kadhaa amewataka
Wakristo nchini Tanzania kutolipiza kisasi kutokana na madhulumu ya kidini wanayokabiliana
nayo nyakati hizi. Lakini anasema, mambo haya hayapaswi kufumbiwa macho kana kwamba,
hakuna kinachoendelea nchini Tanzania. Haki inapaswa kutendeka!