Mwombeni Bikira Maria awafundishe kumwilisha Imani yenu katika matendo!
Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii,
anawaalika kwa namna ya pekee wakati huu wa mwezi wa Rozari Takatifu kumwomba Bikira
Maria, ili aweze kuwafundisha kumwilisha vyema imani yao katika matendo ya kila siku
pamoja na kutoa nafasi zaidi kwa Kristo.