2013-05-03 11:22:12

Mchango wa waamini walei katika kuyatakatifuza malimwengu!


Baba Mtakatifu Francisko, Jumamosi tarehe 4 Mei 2013 anatarajiwa kuongoza Ibada ya Rozari Takatifu kwenye Kanisa kuu la Bikira Maria Mkuu lililoko mjini Roma kuanzia majira ya saa 12:00 Jioni. Jumapili asubuhi ataungana na mashirika ya kitume na vyama vya sala kutoka sehemu mbali mbali za dunia walioko hapa Roma kwa ajili ya Maadhimisho ya Mwaka wa Imani.

Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto wa kumi na sita katika Waraka wake wa kichungaji, Afrcae Munus, Dhamana ya Afrika anabainisha kwamba, kwa njia ya waamini walei, Kanisa limo na linafanya kazi ulimwenguni. Waamini walei wanapaswa kupewa majiundo makini ya maisha ya Kikristo; Kibiblia, Kiroho, Kiliturujia na Kichungaji, ili waweze kweli kuyatakatifuza malimwengu kwa njia ya maisha na utume wao.

Waamini walei wanaitwa kwa namna ya pekee kuwa ni watakatifu, ili waweze kuwa kweli ni chumvi ya dunia na nuru ya ulimwengu. Vyama vya kitume ni majukwaa makini katika mchakato wa kumshuhudia Kristo ulimwenguni. Waamini Walei wanachangamotishwa kujivunia Ukristo wao kwa kutambua mchango wanaoweza kuutoa kwa ajili ya mafao ya wengi na maendeleo endelevu ya binadamu aliyeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu.







All the contents on this site are copyrighted ©.