2013-05-01 09:47:19

Vatican yatuma salam za pongezi kwa Waziri mkuu wa Italia


Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu mkuu wa Vatican amemtumia salam za pongezi Waziri mkuu mpya wa Italia Bwana Enrico Letta kwa kuchaguliwa na hatimaye kupitishwa na Bunge la Italia. Katika mazungumzo baina ya viongozi hawa wawili kwa njia ya simu, wameweza kubadilisha mawazo kuhusu baadhi ya vipaumbele vinavyoweza kufanyiwa kazi nchini Italia na katika ajenda ya Jumuiya ya Ulaya.

Wakati huo huo, Kardinali Angelo Bagnasco, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Italia baada ya Maadhimisho ya Misa Takatifu kwenye Makao makuu ya Benki ya Carige yaliyoko mjini Genova, Siku ya Jumanne tarehe 30 Aprili 2013 amepongeza ziara ya kikazi inayofanywa na Waziri mkuu wa Italia Bwana Enrico Letta kwamba, inapania kurudisha imani kwa nchi ya Italia ambayo kwa sasa inakabiliwa na hali ngumu ya uchumi na kuna kundi kubwa la wanawake na vijana hawana fursa za ajira, jambo ambalo linaendelea kuwakatisha tamaa ya maisha!







All the contents on this site are copyrighted ©.