2013-05-01 08:56:26

Papa mstaafu Benedikto XVI tarehe 2 Mei 2013 anarejea mjini Vatican


Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI anatarajiwa Alhamisi tarehe 2 Mei 2013 majira ya jioni kurejea mjini Vatican na kuendelea na maisha yake kwenye Konventi ya Mater Ecclesiae iliyobuniwa na Mwenyeheri Yohane Paulo wa pili kunako mwaka 1989 na kukamilika kunako mwaka 1992.

Tangu alipong'atuka kutoka madarakani kwa utashi na uhuru kamili kwa ajili ya mafao na ustawi wa Kanisa amekuwa akiishi kwenye Ikulu Ndogo ya Castel Gandolfo iliyoko nje kidogo ya mji wa Roma.

Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI wakati wote huu amekuwa akisali na kutafakari kwa ajili ya Kanisa kama alivyokuwa amesema mwenyewe yapata miezi miwili iliyopita. Padre Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican amethitisha habari hizi na kuongeza kwamba, afya ya Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto wa kumi na sita ni njema, ila tu umri unazidi kumwelemea na kwamba, amedhohofu kidogo!







All the contents on this site are copyrighted ©.