2013-05-01 08:37:38

Mtakatifu Yosefu Mfanyakazi!


Mama Kanisa kila mwaka ifikapo tarehe Mosi, Mei anaadhimisha Kumbu kumbu ya Mtakatifu Yosefu Mfanyakazi, sanjari na Siku ya Wafanyakazi Duniani. Kanisa linatambua na kuthamini umuhimu wa kazi kama wajibu na utimilifu wa mwanadamu na ushiriki wake katika kutiisha dunia pamoja na kutoa huduma kwa Jumuiya ya binadamu.

Mababa wa Mtaguso mkuu wa pili wa Vatican wanasema, huu ni mwendelezo wa ushiriki wa mwanadamu katika kazi ya uumbaji na mpango wa ukombozi.

Kumbu kumbu ya Mtakatifu Yosefu msimamizi wa wafanyakazi, ilianzishwa kunako mwaka 1955 na Baba Mtakatifu Pio wa kumi na mbili. Akaamuru kwamba, siku hii iadhimishwe sanjari na Siku ya Wafanyakazi Duniani, kila mwaka ifikapo tarehe Mosi, Mei.







All the contents on this site are copyrighted ©.