Jifunzeni kutoka kwa Mtakatifu Yosefu ambaye kamwe hakukata tamaa!
Vijana wapendwa, jifunzeni kutoka kwa Mtakatifu Yosefu, aliyekumbana na magumu katika
maisha yake, lakini kamwe hakukata tamaa, kiasi kwamba, akatambua namna ya kuvuka
vizingiti vya maisha!
Ni ujumbe wa Baba Mtakatifu Francisko kwa watumiaji
wa mitandao ya kijamii, twitter wakati huu Jumuiya ya Kimataifa inapoadhimisha Siku
kuu ya Wafanyakazi, kukiwa na bahari ya vijana ambao hawana fursa za kazi, jambo ambalo
linawakatisha tamaa ya maisha!