Zaidi ya Makanisa 70 yamechomwa moto nchini Nigeria!
Kinzani za kiuchumi, kijamii, kisiasa na kidini nchini Nigeria, zimepelekea zaidi
ya Makanisa 70 kuchomwa motokwenye Jimbo la Benue, Kati kati mwa Nigeria, kiasi kwamba,
kuna maelfu ya waamini hasa wale wanaoishi vijijini hawana tena nyumba za Ibada.
Hayo
yamo kwenye taarifa kutoka kwenye Tume ya haki, amani na maendeleo ya Jimbo Katoliki
Makurdi. Kuna idadi kubwa za shule za msingi na sekondari ambazo zinamilikiwa na Makanisa
nchini Nigeria zimechomwa pia moto katika miezi ya hivi karibuni.
Kinzani
za kikabilia na kati ya wakulima na wafugaji nchini Nigeria zimepekea maafa makubwa
kwa maisha na mali za watu. Mapigano haya wakati mwingine yamekuwa ni makali kutokana
na silaha za moto zinazotumika hali ambayo inaonesha kwamba, kuna silaha nyingi ambazo
zinamilikiwa kinyume cha sheria za nchi na hivyo kuhatarisha amani na usalama wa wananchi
wa Nigeria.
Viongozi wa Makanisa nchini Nigeria wanaitaka Serikali kusimama
kidete kulinda na kutetea maisha na mali ya raia wake na kwamba, sheria ichukue mkondo
wake kwa wote wanaobainika kwamba, wanaleta vurugu nchini humo.