2013-04-29 11:13:28

Mawaziri Italia wala kiapo wakati damu ya Askari Polisi ikimwagika nje ya Ikulu!


Baraza la Mawaziri nchini Italia lenye Mawaziri 21, linaloongozwa na Waziri mkuu mpya Bwana Enrico Letta, Jumapili tarehe 28 Aprili 2013, limekula kiapo cha utii kwa Jamhuri, wakati ambapo Jeshi la Polisi lilikuwa likipambana na Bwana Luigi Preiti aliyeingia kwenye eneo la tukio akiwa na lengo la kuwafyatulia risasi wanasiasa lakini kwa bahati mbaya, risasi hizi zikawapata Askari wawili waliokuwa kwenye ulinzi.

Kati yao Askari mmoja amefanyiwa upasuaji mkubwa na hali yake bado si nzuri. Viongozi mbali mbali wa Serikali na Vyama vya Kisiasa nchini Italia vimeshutumu sana kitendo hiki ambacho kimevuruga amani na utulivu wakati wa sherehe za kula kiapo kwa Baraza la Mawaziri la Italia.

Kardinali Angelo Bagnasco, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Italia anabainisha kwamba, hili ni onyo kwa wanasiasa kwani inaonekana kwamba, watu wengi wamekata tamaa kutokana na athari za myumbo wa uchumi kimataifa na kwamba, wanasiasa wanapaswa kutoa kipaumbele cha kwanza kwa mafao ya wengi badala ya kujitafuta wao wenyewe na matokeo yake ni vitendo vya kukata tamaa ambavyo wananchi wamekuwa wakivionesha kwa sasa.







All the contents on this site are copyrighted ©.