Papa awapongeza watanzania kwa kusherehekea miaka 49 ya Jamhuri ya Muungano
Baba Mtakatifu Francisko amemtumia salam za matashi mema Rais Jakaya Mrisho Kikwete
wa Tanzania, katika Maadhimisho ya Kumbu kumbu ya Miaka 49 ya Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania. Baba Mtakatifu anawatakia watanzania wote heri, baraka, amani, ustawi
na maendeleo hasa wakati huu anapoanza utume wake kama Khalifa wa Mtakatifu Petro.
Viongozi
kadhaa kutoka Jumuiya ya Kimataifa wameungana na watanzania katika Maadhimisho ya
Miaka 49 ya Muungano wa Tanzania. Kauli mbiu ambayo imeongoza Maadhimisho ya Mwaka
huu ni "Amani, utulivu na maendeleo ni matokeo ya Muungano".