2013-04-26 10:20:50

Kikosi kazi cha Jeshi la Kimataifa kinashutumiwa kwa kuhusika na mauaji ya kinyama Kaskazini mwa Nigeria


Mauaji ya kutisha yaliyotokea hivi karibuni Kaskazini mwa Nigeria kwa kupelekea watu 185 kupoteza maisha yao, kitendo ambacho kilishutumiwa na Jumuiya ya Kimataifa yalisababishwa na operesheni maalum iliyofanywa na Kikosi Kazi cha Jeshi la Kimataifa linaloundwa na wanajeshi kutoka: Nigeria, Chad, Niger na Cameroon waliopewa dhamana ya kulinda usalama kuzunguka Ziwa Chad.

Kikosi hiki kimeshutumiwa vikali kwa kutumia nguvu kupita kiasi kujibu mashambulizi yaliyoelekezwa kwao kutoka kwa Kikundi cha Boko Haram. Mashahidi wanasema kwamba, wanajeshi waliamua kufanya oporesheni hii baada ya kuona kwamba, kuna baadhi ya wananchi waliokuwa wanatoa hifadhi kwa wanajeshi wa Kikundi cha Boko Haram. Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria ameamua kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini ukweli wa mambo.







All the contents on this site are copyrighted ©.