2013-04-25 15:02:26

Mikutano juu ya Kipaimara yawasilishwa Vatican


Katika mazingira ya Mwaka wa Imani, Jumatano , Askofu Mkuu Rino Fischella, Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya ukuzaji wa Uinjilishaji Mpya, aliwasilisha matukio mawili, kwanza ni mkutano wa muda wa siku mbili 27 -28 Aprili juu ya Sakramenti ya Kipaimara, na tukio la pili Siku ya udugu na matendo ya Huruma, hapo tarehe 3-4 Mei.

Katika mahojiano na Fausta Speranza wa Radio Vatican , Askofu Mkuu Rino Fischella, amethibitisha kwamba, Papa Francisko, ameridhia matukio yote yaliyopitishwa na Papa Benedikto XVI, katika wazo lake la kuwa na Mwaka wa Majitolea na Imani. Hivyo tukio lijalo ni kwa ajili ya wale watakaopata daraja la Kipaimara kwa mwaka huu wa 2013. Tayari idadi ya watakao pokea Sakramenti ya Kipaimara inatajwa kuwa elfu sabaini (70,000) lakini kuna mwelekeo wa idadi hiyo kuongezeka.

Na kwamba Papa Francisko atatoa Sakramenti ya Kipaimara kwa wafuasi wa Kristu, wapatao 44 watakao toka Bara mbalimbali za dunia, wengi wao wakiwa vijana. Pia katika kundi la watu wazima, mmoja wao ni kutoka Cape Verde, mwenye umri wa miaka 55. Na wengine watatoka katika makundi mbalimbali ya kijamii akiwemo kijana mlemavu, mwingine atatoka katika eneo lililokumbwa na tetemeko la aridhi lakini wote katika ujumla wao, wanakuwa ni ushuhuda halisi wa umoja wa Kanisa la ulimwengu.








All the contents on this site are copyrighted ©.