2013-04-24 09:03:49

Sababu za Kiuchumi zaongeza uhafidhini Syria


Padre Pierrabattista Pizzaballa, Mkuu wa Jumuiya ya Wafransikani, yenye dhamana ya Ulinzi katika maeneo Matakatifu katika Nchi Takatifu, hivi karibuni ilitoa wito nguvu kwa ajili ya ufumbuzi wa mgogoro wa Syria. ,
Akihojiwa na Redio Vatican,juu ya mgogoro huo na utekwaji wa nyara wa Maaskofu wawili, ameonyesha imani yake kwamba, utekwaji nyara wa Maaskofu hao wawili, wa Kanisa la Kiotodosi , kimsingi umemotisha na sababu za kiuchumi. Maaskofu waliotekwa nyara ni wa eneo la Aleppo, Askofu Mar Gregorios Ibrahim wa Kanisa la Kiotodosi Syria na Askofu Paul Yazigi wa Kanisa la Kiotodosi la Kigriki la Antokia. Na dreva wao aliuawa wakati wao wakiendelea kutoa huduma za kibinadamu wa wahitaji Syria.
Padre Pizzaballa, anasema, kwa bahati mbaya, pamoja na vita vinavyoendelea, pia kuna aina nyingi za magenge na makundi ya wahalifu ambao wanautumia mwanya wa machafuko kujinufaisha kwa namna moja au nyingine , kama pia inavyoonekana Iraq. Na pia sababu za kidini au ushabiki wa kupindukia , haziwezi kuondolewa, lakini hasa zaidi ya yote ni sababu za kiuchumi.
Na akizungumzia matumaini ya jumuiya yake katika kupata jawabu la kusitisha ghasia katika taifa la Syria, aliitaja jumuiya ya kimataifa kwamba, itaweza kusitisha upelekwaji wa silaha na utoaji wa ruzuku kwa waasi na serikali,kigezo kikubwa kinachoendeleza ghasia hizo siku hadi siku.
Aliendelea kugusia madhara makubwa ya kiuchumi yaliyosababishwa na matokeo ya vita vya wenyewe, yaliyovuka hata mipaka ya Syria na kuingia katika nchi jirani, ambako mamilioni ya Wasyria wanaishi kama wakimbizi. Watu hao wamepoteza matumaini ya kuajiriwa, mbele yao kumefunikwa na giza nene dhidi ya ajira, licha ya kukosa makazi na mahitaji ya msingi.
Na hivyo , pamoja na wakimbizi, pia kuna waasi, na wahafidhina, wanaoeneza kama moto nyikani, uzushi wa kila aina, ambayo kwa bahati mbaya umeshuhudiwa pia katika taifa la Iraq na mahali pengine Mashariki ya Kati.

Padre Pizza balla alimalizia maelezo yake na matumaini ya kibiblia. Na kwamba, ni muhimu kwa Wakristo kutoihama Syria , bali wabaki na imani hai katika kuitetea imani yao kwa nchi alimozaliwa Yesu Kristu







All the contents on this site are copyrighted ©.