2013-04-23 08:02:09

Wanasiasa wa Italia wanapaswa kuwajibika kwa ajili ya mafao ya wengi!


Rais Giorgio Napolitano baada ya kula kiapo na kulihutubia Bunge la Italia, hapo tarehe 22 Aprili 2013 anakuwa ni Rais wa kumi na mbili ambaye amebahatika kuiongoza Italia kwa vipindi viwili, jambo ambalo halijawahi kutokea katika historia ya Italia.

Rais Napolitano mwenye umri wa miaka 88 katika hotuba yame anawataka wanasiasa wa Italia kutekeleza wajibu wao kikamilifu wakizingatia nidhamu, umoja wa kitaifa na mafao ya wengi ili kuwajengea tena matumaini mapya wananchi wa Italia ambao wanaendelea kukata tamaa kutokana na athari za myumbo wa uchumi kimataifa pamoja na kinzani za kisiasa.







All the contents on this site are copyrighted ©.