Haiwezekani kudai kuishi na Kristu na huku uko nje ya Kanisa- Papa
Jumanne hii 23 Aprili, maelfu ya salaam za matashi mema zimemiminika kwa Papa Francis,
kwa ajili ya adhimisho la Siku Kuu ya wajina wake Mtakatifu George. Papa Francis,
jina lake jingine ni George Mario Bergoli. Kwa ajili ya Siku Kuu hii, Mapema
Jumanne, Papa aliadimisha Ibada ya Misa Katika kikanisa cha Mtakatifu Paulo cha mjini
Vatican , akiwa na Makardinali wanaoishi Roma. Katika Ibada hiyo, Papa aliwashukuru
Makardinali kwa kushirikiana nae katika adhimisho hili na kwa mapokezi na ukaribu
wao, wanaounyesha tangu alipochaguliwa kuwa Papa 19 March mwaka huu. Alisema, anajisikie
vyema kuwa karibu nao. Akizungumza juu ya masomo ya siku, aliireja ari ya wakristu
wa mwanzo katika kuieneza Injili, licha ya kukabiliana na katika kipindi cha mateso
yaliyotaka kuvunja asili ya utume wa kimisionari wa Kanisa" wa kuieneza Injili katika
maeneo ya Foinike, Kupro na Antiokia. Wakristu hao wa mwanzo, walijawa na ari ya
kitume, na imani ni hivyo kutawanyika huko na kule wakiitangaza Injili. Somo la Injili
lililoonyesha, ndivyo ilivyokuwa pia kwa Wayunani, na wapagani. Ilikuwa ni hatua
makini kufanikisha mpango wa Roho Mtakatifu.