Salaam za Matashi Mema ya Papa Francesco kwa Rais Mpya wa Italia
Jumamosi mara baada ya Rais Giorgio Napolitano, kuchaguliwa tena kuwa Rais wa Jamhuri
ya Italia, Papa Francesco, alipeleka salaam zake za matashi mema kwa Rais huyo kwa
njia ya telegram. Papa Francesco, katika salaam hizo ameonyesha heshima na shukurani
zake za dhati kwa Rais Giogio Napolitano, kuchaguliwa tena kuliongoza Taifa la Italia
kisiasa. Na pia ameonyesha matumaini yake kwamba, ataendelea kutembea katika mwanga
wa busara na ushirikiano mzuri na wakuu wote, katika huduma yao kwa kila binadamu
na taifa pendwa la Italia. Na mwisho alitoa baraka zake za kitume, akimtakia
moyo wa kujenga mustakabali wa maelewano, mshikamano na tumaini jema.