2013-04-22 15:06:08

Papa ahimiza sala za kuombea Miito duniani kote.


Yesu anachokitaka kutoka Kwenu : Ni kuwa wachungaji wenye huruma na si watendaj, Papa amewaasa Mapadre wapya.
Jumapili iliyopita, ambayo ilikuwa ni Adhimisho la 50 la Siku ya Dunia ya Kuombea Miito duniani , adhimisho lililoongozwa na Mada Kuu” Miito alama ya Tumiani lililosimikwa katika Imani “, Papa Francisko, aliongoza Ibada ya Misa ambamo alitoa daraja la Upadre kwa waseminaristi kumi wa Jimbo la Roma. Ibada hiyo ilifanyika katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, majira ya asubuhi.
Mapadre hao ni wahitimu kutoka Seminari Kuu ya Jimbo la Roma , Seminari inayosimamiwa na Jumuiya ya Njia ya Ukatukumeni Mpya , Mama wa Mkombozi na Seminari ya Upendo Mtakatifu.
Papa Francesco, katika homilia ya wakati wa kuwaweka wakfu Mapadre wapya, alielenga zaidi katika moja ya misingi ya ukuu wa Papa kama Askofu wa Jimbo la Roma, katika Upadirisho huo. Na aliendelea kutafakari juu ya sakramenti ya Upadre akisema muda si mrefu watakuwa wakiwahudumia watu wa Mungu kama Makuhani Wakuu wa Kristu , na hivyo aliwataka daima kuwa wachungaji wenye huruma kwa watu na si tu kuwa wasimamizi au mameneja. .

Mandhari ya miito, ilitawala katika hotuba za Papa alizozitoa hata baadaye wakati wa Sala ya Malkia wa Mbungu, iliyohudhuriwa na watu wanao kadiriwa kufikia 70 elfu, waliokusanyika katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, majira ya saa sita za mchana. .

Papa Francesco, alibainisha kuwa "wakati mwingine Yesu anatuita na anatualika kumfuata, lakini inaweza kutokea, tukashindwa kumtambua kuwa Yeye Yesu. Na hivyo alihimiza waumini na hasa vijana kuisikiliza kwa makini sauti ya Kristo katikati katika mawazo, na hasa katika harakati za maisha yanayotaufa ukweli adilifu. Aliwasihi vijana kwa ujasiri, kumsikiliza Bwana.


Pia alibainisha kuwa "nyuma na mbele ya kila wito wa ukuhani au maisha ya wakfu, daima husindikizwa na nguvu ya maombi, iwe kutoka kwa mtu binafsi, bibi, babu, mama, baba, shangazi au jamii ya waumini kwa ujumla ". Sala inayoomba waamini kila mahali kuongeza juhudi zaidi katika kuombea Miito , ambayo hata leo hii, ni hitaji muhimu, ili wafanyakazi katika shamba la Bwana, waweze kuongezeka.








All the contents on this site are copyrighted ©.