2013-04-22 15:12:40

Mwana Mazingira ajenga tumaini kwa Papa Francisko


Tarehe 22 Aprili 2013, dunia inafanya adhimisho la 43 la Siku ya Mazingira Duniani , adhimisho linalo wahusisha zaidi ya watu bilioni moja duniani kote. Ni maadhimisho ya kila mwaka, yenye kuonyesha utendaji mbalimbali, kwa ajili ya kuonyesha utetezi na ulinzi mazingira.

Papa Francis , hapo tarehe 19 March mwaka huu, akitoa hotuba yake ya kwanza mara baada ya kuchaguliwa kama Papa , alionyesha kujali umuhimu wa kutetea na kutunza mazingira katika asili yake. Hoja iliyogusa watetezi na walinzi wote wa viumbe na mazingira asilia.
Aliwatahadharisha wote wale wenye nafasi za uongozi, iwe kisiasa, kiuchumi, au kijamii, wake kwa waume wenye mapenzi mema, kuwa watetezi na walinzi wa viumbe, walinzi wa mpango wa Mungu, ulio andikwa katika asili yote, walinzi wa mmoja kwa mwingine na mazingira ".

Adhimisho la mwaka huu la Siku ya Dunia 2013 linaoongozwa na Kaulimbiu : "uso wa Mabadiliko ya Tabianchi", na imechaguliwa kwa lengo la kutoa angalisho makini zaidi , katika athari zinazo zidi kuleta mabadiliko katika tabia nchi , kama inavyoshuhudiwa na mtu binafsi na dunia kwa ujumla.

Adhimisho hili huratibiwa na Asasi ya Mtandao wa Siku ya Dunia, kwa kushirikiana na wabia wengine katika kazi za kutetea na kudumisha mazingira bora duniani, Asisi inayoongozwa na Rais Bibi Kathleen Rogers.
Bibi Rogers mapema Jumanne, akizungumza katiak mahojiano na Linda Bordoni wa Redio Vatican, alionyesha tumaini lake kubwa, alilolijenga kwa Papa Francesco,katika kupambana na athari za mabadiliko ya tabia nchi na ulinzi wa dunia na viumbe wake. Amesema,”Hotuba ya kwanza ya Papa Francesco, ili ashiria mengi, juu ya mazingira asilia ya dunia na wanyama. Na pia, uzoefu wake, yeye mwenyewe katika kuyaishi maisha ya kawaida , kama kutumia usafiri wa umma, kujipikia mwenyewe, na maisha yake ya kawaida, yanaoonyesha kwamba, kila mtu anaweza kuziishi nyayo hizo za maisha ya kawaida lakini endelevu. Bi Rogers, aliendelea kuionyesha imani yake kwa Papa Francesco kwamba, kwa ukuu wa nafasi yake, anao uwezekano wa kuiongoza dunia katika utendaji wa kidharura kwa ajili ya kuikoa dunia dhidi ya shinikizo la kidharura za mabadiliko ya tabia nchi, kwa sababu kila mtu humsikiliza.

Anaamini Papa Francesco , anao uwezo kuchukua jukumu hili kubwa kwa kuwa yeye mwenyewe anajali maskini, na tayari ana wasiwasi kuhusu athari za mabadiliko ya tabia nchi yanavyo lemea watu maskini, na hasa katika muono kwamba, tayari aliyaishi maisha hayo na hivyo anaizungumzia hali aliyoiishi katika maisha yake ya kila siku, kama pia ambavyo tayari, anafahamika kuwa mtetezi mashuhuri katika masuala ya usawa wa kijinsia, na viongozi wa serikali na mashirika humsikiliza.








All the contents on this site are copyrighted ©.