Balozi wa Falme za Kiarabu akutana na Papa Francisko
Baba Mtakatifu Francisko, Jumatano tarehe 17 Aprili 2013 mara baada ya Katekesi yake
kwa mahujaji na wageni kutoka sehemu mbali mbali, alikutana na kuzungumza na Bwana
Saleh Mohammad Al Ghamdi, Balozi wa Falme za Kiarabu nchini Italia aliyewakilisha
ujumbe maalum kwa Baba Mtakatifu Francisko kutoka kwa Mfalme Abdullah Bin Abdulazizi
Al Saud.