Maelfu ya mashabiki wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza kati ya mwaka 1979 hadi
1990, Magaret Thatcher, mapema Jumatano hii, walimiminika katika Kanisa kuu la Westminster
, mjini London, kuhudhuria ibada ya wafu na maziko ya Waziri Mkuu huyo. Margret Thatcher
, alifariki Jumatatu ya tarehe 8 April, kwa maradhi ya kiharusi. Malkia wa Elizabeth
11, alikuwa kati ya wanasiasa mashuhuri wa Uingereza na kutoka pande mbalimbali za
dunia waliohudhuria Ibada na mazishi hayo. Asubuhi na mapema, maelfu ya watu
walijipanga katika mitaa ya jiji la London ambako jeneza la Marehemu Margaret Thatcher,
likiwa limebebwa katika gari maalum la farasi , lilipitishwa kwa heshima zote za taifa
la Uingereza ,kuelekea katika Jengo mashuhuri la Kisiasa nchini Uingereza, kukamilisha
safari yake ya kabla ya mazishi. Mabango mengi yaliyokuwa yamebebwa , yalikuwa na
maneno ya sifa kwa Margaret Thatcher , ingawa pia kulikuwa na wachache waliomkashifu.
Na wengi waliohojiwa kuhusu maziko haya wameonyesha kutofurahishwa na matumizi
ya dola millioni 15 za Marekani za walipa kodi , kutumika katika mazishi haya ya
kifahali. Margaret Thatcher amepewa heshima ya kuangwa kwa mlio wa bunduki uliosikika
kila dakika tokea mnara wa London, na mlio wa kengere kubwa ya jiji hilo. Katika
kipindi cha miaka 150, Marehemu Margaret Thatcher, anakumbukwa katika historia ya
Uingereza, kuwa mwanamke wa kwanza kutumikia kwa muda mrefu kama Waziri Mkuu wa Uingereza.
Na aliweza kufanikisha mengi , ikiwemo ushindi wa ejshi la Uingereza latola vota ya
Falklands ya mwaka 1982.