Imegota miaka 86 tangu alipozaliwa Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI
Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto wa kumi na sita, tarehe 16 Aprili 2013 anaadhimisha
kumbu kumbu ya miaka 86 tangu alipozaliwa. Papa mstaafu Benedikto wa kumi na sita
kwa sasa bado anaendelea kuishi Ikulu Ndogo ya Castel Gandolfo, iliyoko nje kidogo
ya Mji wa Roma.
Tangu alipong'atuka kutoka madarakani amekuwa akitumia muda
wake mrefu kwa ajili ya kusali, kutafakari, kujisomea vitabu pamoja na kusikiliza
muziki. Watu wengi wanamkumbuka kutokana na ujasiri wake aliouonesha kwa kung'atuka
kutoka madarakani kwa uhuru na utashi kamili, ili kutoa nafasi kwa ajili ya kiongozi
mwingine atakeendeleza dhamana ya kuliongoza Kanisa kwa ari na moyo mkuu.