Papa Francisko aguswa na mateso ya wananchi wa Iran waliokumbwa na tetemeko la ardhi
Baba Mtakatifu Francisko wakati wa Katekesi yake, Jumatano tarehe 10 Aprili 2013,
ameonesha masikitiko na mshikamano kwa wananchi wa Iran ambao, Jumanne tarehe 9 Aprili
2013 walikumbwa na tetemeko la ardhi lililosababisha maafa makubwa katika maisha na
uharibifu wa miundo mbinu. Baba Mtakatifu anawaombea wote waliofariki dunia na majeruhi
anawatakia uponaji na afya njema na kwamba, anawakumbuka wote waliofikwa na maafa
haya.
Taarifa kutoka katika vyombo vya habari inaonesha kwamba, hadi kufikia
Jumatano tarehe 10 Aprili 2013 asubuhi zaidi ya watu 40 walikuwa wamekwisha poteza
maisha na wengine 850 wamejeruhiwa vibaya katika mji wa Dashti, nchini Iran. Miundo
mbinu mingi imeharibiwa kwenye Kijiji cha Chahgah, kilichoko karibu na mji wa Dashti.