Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii maarufu
kama twitter, jumapili iliyopita anasema, inapendeza kumwona Yesu akiwaangalia wafuasi
wake, ni uso unaofariji. Anawataka waamini kutoikatia tamaa huruma na uvumilivu wa
Mungu. Itakumbukwa kwamba, Jumapili iliyopita, Mama Kanisa ameadhimisha Jumapili ya
Huruma ya Mungu.