Maadhimisho ya Siku ya Mtoto Asiyezaliwa, tarehe 8 Aprili 2013
Shirika la kutetea uhai Tanzania, "Pro Life Tanzania" tangu mwaka 2002 limekuwa likiadhimisha
Siku ya kutetea uhai. Kunako mwaka 2007 Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania likatangaza
kwamba, Domenika kabla ya Siku kuu ya Bikira Maria kupaswa habari kuwa atakuwa Mama
wa Mungu, iadhimishwe kitaifa siku ya mtoto asiyezaliwa.
Hii ni siku
ya kukumbuka maajabu ya Mungu ili kusimama kidete kulinda, kutetea na kuenzi Injili
ya Uhai dhidi ya utamaduni wa kifo. Kwa mwaka huu, Siku kuu ya Bikira Maria kupashwa
habari inafanyika, Jumatatu tarehe 8 Aprili 2013
Ifuatayo ni tafakari ya kina
iliyotolewa hivi karibuni na Ndugu Emil Hagam, Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la kutetea
uhai Tanzania, kama inavyosomwa kwako ndani ya Studio za Radio Vatican na Padre George
wa Bodyo.