Cor Unum yatoa msaada kwa waathirika wa mafuriko nchini Argentina
Baraza la Kipapa linaloratibu misaada ya Kanisa Katoliki, Cor Unum, kwa niaba ya Baba
Mtakatifu Francisko, limetuma kiasi cha dolla za kimarekani 50,000 ili kusaidia juhudi
za kuokoa maisha ya watu waliokumbwa na mafuriko makubwa hivi karibuni Jimboni La
Plata, Argentina.
Hiki ni kielelezo cha mshikamano wa upendo na watu walioathirika
kutokana na mafuriko hayo ambayo yamesababisha maafa makubwa na uharibifu wa miundo
mbinu. Shirika la Misaada la Kanisa Katoliki Argentina liko mstari wa mbele kusaidia
kutoa msaada wa dharura kwa watu walioathirika zaidi.