Papa Francisko atuma ujumbe wa mshikamano na wananchi wa Argentina waliokumbwa na
mafuriko
Baba Mtakatifu Francisko ametuma salam za rambi rambi kwa wananchi wa Argentina waliokumbwa
na mafuriko makubwa mjini Buenos Aires, yaliyopelekea zaidi ya watu 60 kupoteza maisha
na maelfu ya watu kukosa mahali pa kuishi pamoja na miundo mbinu mbali mbali kuharibiwa
vibaya.
Ujumbe wa Baba Mtakatifu Francisko umeandikwa kwa niaba yake na Kardinali
Tarcisio Bertone, Katibu mkuu wa Vatican kwenda kwa Askofu mkuu Mario Aurelio Poli
wa Jimbo kuu la Buenos Aires. Baba Mtakatifu anasema, anapenda kuwaonesha mshikamano
wake wa dhati wakati huu wanapokabiliana na hali ngumu ya maisha. Anawaalika waamini
na watu wenye mapenzi mema kuonesha mshikamano wa upendo na wote walioathirika kwa
kuwapatia msaada wa hali na mali.