18 wamenusurika kwenye ajali ya Jengo Dar es Salaam
Taarifa ya Shirika la Habari la Reuters inaonesha kwamba, hadi kufikia tarehe Mosi
Aprili 2013, idadi ya watu waliofariki dunia kutokana na kuangukiwa na ghorofa Jijini
Dar es Salaam kwa sasa imefikia watu 36.
Juhudi za kuendelea kufukua kifusi
kwa matumaini ya kupata miili mingine iliyofukiwa sehemu hii yanazidi kufifia kila
siku. Taarifa ya Jeshi la Polisi inaonesha kwamba, kuna watu 18 walionusurika kwenye
ajali ya kuporomoka kwa Jengo lenye ghorofa 16 kati kati ya Jiji la Dar es Salaam.