Baba Mtakatifu Francisko katika maadhimisho ya Siku kuu ya Pasaka kwa Mwaka 2013,
anawaalika kwa namna ya pekee kabisa, watumiaji wa mtandao wa twitter kumkubali na
kumpokea Yesu Kristo Mfufuka katika maisha yao. Hata kama wanajisikia kuwa wako mbali,
wajitahidi kupiga moyo konde na kuanza kuchukua hatua ya kumwelekea Yesu ambaye amefumbua
mikono yake, tayari kuwapokea kwa mikono miwili.