2013-03-31 11:24:23

Hali ni shwari, baada ya watu wawili kupoteza maisha Kisumu!


Watu wawili wamepoteza maisha mjini Kisumu, baada ya Mahakamu kuu ya Kenya, Jumamosi jioni tarehe 30 Machi 2013 kutangaza kwamba, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, alikuwa amechaguliwa kwa kura halali. Vifo hivi vimetokea mjini Kisumu inayosadikiwa kuwa ni ngome kuu la Raila Odinga aliyekuwa amekata rufaa Mahakama kuu kupinga uchaguzi mkuu wa Rais.

Vijana na washabiki wa Raila Odinga hawakufurahia na uamuzi wa Mahakama kuu na hivyo wakajikuta wanakabiliana uso kwa uso na vikosi vya kutuliza ghasia nchini Kenya. Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya, limeendelea kuwataka wananchi wa Kenya kulinda na kudumisha amani na utulivu kama kikolezo cha maendeleo endelevu. Machafuko ya kisiasa yaliyojitokeza kunako mwaka 2007 liwe ni onyo kali kwa wanasiasa na wananchi wanaotaka kuitumbukiza tena Kenya katika machafuko ya kisiasa.

Taarifa ya Jeshi la Polisi siku ya Jumapili asubuhi ilionesha kwamba, amani na utulivu vimerudi tena kwenye maeneo ambayo yalionekana kuwa na cheche za vurugu za kisiasa.







All the contents on this site are copyrighted ©.