Baba Mtakatifu Francisko katika Maadhimisho ya Alhamis Kuu, Siku ambayo Mama Kanisa
anakumbuka kwa namna ya peke, Yesu alipoweka Sakramenti ya Ekaristi Takatifu, Daraja
Takatifu na Huduma ya Upendo, anawaalika watumiaji wa mtandao wa twitter, kuwa karibu
na Mapadre wao kwa njia ya upendo na sala, ili daima waweze kuwa ni wachungaji kadiri
ya moyo wa Kristo.