Ratiba elekezi ya Maadhimisho ya Juma kuu mjini Vatican yatakayomshikirikisha Baba
Mtakatifu Francisko
Mshereheshaji mkuu wa Ibada za Kipapa, Monsinyo Guido Marini anasema kwamba, Ratiba
ya Maadhimisho ya Ibada za Juma kuu zitakazoongozwa na Baba Mtakatifu Francisko zitakuwa
kama ifuatavyo:
Tarehe 28 Machi 2013: Alhamisi kuu, Saa 3:30 Asubuhi, Baba
Mtakatifu ataongoza Ibada ya Misa ya Kubariki Mafuta Matakatifu, itakayofanyika kwenye
Kanisa kuu la Mtakatifu Petro, mjini Vatican. Mafuta yatakayobarikiwa kwa ajili ya
matumizi ya Ibada Jimbo kuu la Roma yataweza kupatikana kutoka kwenye Sakristia ya
Kanisa kuu la Mtakatifu Yohane wa Laterano.
Tarehe 29 Machi 2013: Ijumaa kuu,
Saa 11: 00 Jioni; Siku ya Kumbu kumbu ya Mateso ya Yesu Kristo. Baba Mtakatifu Francisiko,
atashiriki katika Ibada ya Liturujia ya Neno, Kuabudu Msalaba na Kupokea Ekaristi
Takatifu, kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro, mjini Vatican
Tarehe 29 Machi
2013, Ijumaa kuu, Usiku saa 3:15: Baba Mtakatifu Francisko ataadhimisha Ibada ya Njia
ya Msalaba kuzunguka Magofu ya Coloseo. Itakumbukwa kwamba, tafakari ya Njia ya Msalaba
kwa Mwaka 2013 inatolewa na Kardinali Bèchara Boutros Rai, Patriaki wa Kanisa la Wamaroniti
kutoka Antiokia. Tafakari hii ni kilio dhidi ya kila aina ya ukosefu wa haki msingi
za binadamu; ni mwaliko wa kutafakari kutoka katika dimbwi la kifo na kuanza hija
ya maisha mapya.
Tarehe 30 Machi 2013: Kesha la Siku kuu ya Pasaka litaanza
hapo saa 2:30 kwa Baba Mtakatifu Francisko kubariki moto na baadaye kuingia ndani
ya Kanisa kuu la Mtakatifu Petro kwa maandamano yatakaoongozwa na Mshumaa wa Pasaka,
alama ya Kristo Mfufuka. Kanisa litaimba Mbiu ya Pasaka kutangaza sifa za mshumaa
wa Pasaka. Itafuata Liturujia ya Neno la Mungu, Ibada ya Ubatizo pamoja na Ibada ya
Ekaristi Takatifu.
Tarehe 31 Machi 2013 Siku kuu ya Pasaka: Baba Mtakatifu
Francisko anatarajia kuanza Ibada ya Pasaka saa 4:15 Asubuhi. Baada ya Maadhimisho
haya, atatoa Salam kwa Mji wa Roma na Dunia kwa ujumla, kama zinavyojulikana kwa Lugha
ya Kilatini, Urbi et Orbi.
Kwa sasa hii ndiyo Ratiba Elekezi iliyotolewa na
Mshehereshaji Mkuu wa Ibada za Kipapa, Monsinyo Guido Marini. Idhaa ya Kiswahili ya
Radio Vatican, itakuwa nawe bega kwa bega ili kukujuza yale yatakayojiri katika Ibada
hizi, unaweza pia kufuata matangazo haya kwa kutumia tovuti ya Radio Vatican kwa anuani
ifuatayo: