2013-03-22 07:51:37

Utunzaji bora wa mazingira unapania kuenzi zawadi ya maisha!


Wakati wa kusimikwa kwake kama Askofu mkuu wa Jimbo la Roma, hapo tarehe 19 Machi 2013, Baba Mtakatifu Francisko amekumbusha tena kwamba, uongozi ni huduma kwa ajili ya: maskini: kiroho na kimwili; wanyonge na wale wanaosukumizwa pembezoni mwa Jamii. Lengo ni kupania kutokomeza mambo yote yanayoendelea kusababisha umaskini, njaa na maradhi. RealAudioMP3

Hapa kuna haja ya kujenga mshikamano wa dhati unaosimamiwa na kanuni auni. Ni tukio ambalo lilihudhuriwa na wakuu wa nchi na wawakilishi wa Serikali zaidi ya 132, changamoto ni kuendelea kusimamia haki jamii, amani na utunzaji bora wa mazingira.

Katika mahojiano maalum na Radio Vatican wakati Waziri mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda na ujumbe wake walipotembelea Studio za Radio Vatican, Mheshimiwa Christopher Mvula, kaimu Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani na Mwakilishi wa Tanzania mjini Vatican anasema, ujumbe uliotolewa na Baba Mtakatifu Francisko ni changamoto ya Kanisa kuendelea kushikamana na maskini kwa kuwajali na kuwasaidia katika mahitaji yao msingi.

Anasema, utunzaji bora wa mazingira ni changamoto endelevu kwa Jumuiya ya Kimataifa kutoka na madhara makubwa yanayosabanishwa na athari za mabadiliko ya tabia nchi sehemu mbali mbali za dunia. Utunzaji bora wa mazingira unapania kuenzi zawadi ya maisha.








All the contents on this site are copyrighted ©.