2013-03-22 16:01:32

Rufaa ya Makanisa ya Oceania kwa haki za Kijamii na uadilifu wa uumbaji


Baraza la Makanisa la Kiekumene la Oceania Pacific, (PCC) katika mkutano wake wa kumi, ulio malizika hivi karibuni mjini Honiara, limetoa wito na rufaa kwa watu wote, kujali na kuheshimu haki za binadamu na ulinzi wa mazingira.
Tamko kutoka Baraza hili lenye kujumuisha jumuiya za kidini 34 , lililonukuliwa na gazeti la L'Osservatore Romano, ambamo wajumbe wa Baraza wametoa wito kwa mamlaka za kimataifa, kutumia njia zote muhimu, kukuza maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kiutamaduni kwa watu asilia, ikiwemo ulinzi na usalama wa mazingira unaowekwa hatarini na mabadiliko ya hali ya hewa yanayo endelea. Miongoni mwa masuala kushughulikiwa yenye kuleta madhara katika mazingira na watu, ni majaribio ya kijeshi yanayotumia silaha ya nyuklia, yanayo fanywa katika baadhi ya maeneo ya Pacific.
Jumuiya za kidini zimetoa wito wa kudai fidia kwa uharibifu unao fanyika. Wajumbe katika mkutano pia alielezea tatizo la uchafuzi unaofanywa na mitambo ya machimboya madini, na kuzitaka serikali katika mkoa huo wa Pacific, kuwa na mshikamano na watu ambao wanakabiliwa na athari hazi, zinazotokana na shughuli za madini,hasa katika mazingira ya baharini. Pia wametaja matatizo yanayo sababishwa na wavuvi wa kimataifa kutoka nje,ambao wameonyesha kutojali uharibifu wanaoufanya isipokuwa kutafuta faida zao binafsi. Watu wa Pacific wanakemea uharibifu huo waksiema, ni kuyaharibumaisha ya watu katiakmkoa huo kwa kuwa mazingira ya bahari ni chanzo kikuu cha chakula na ustawi wake kiuchumi.
Mwisho wamependekeza ukuzaji wa heshima kwa utu wa watu walioambukizwa virusi vya ukimwi, na pia utoaji wa msaada kwa watu walio yahama makazi yao, wakikimbia hatari za vurugu za utumiaji wa silaha zinazo shamirishwa na kuenea kwa silaha, toka nje.

Wajumbe wa Baraza hili pia waliutumia muda wa mkutano huo, kutoa michango na tafakari na kupendekeza mada za kupelekwa katika Mkutano Mkuu wa Baraza la Makanisa Ulimwenguni (WCC) utakaofanyika wakati wa kipindi cha vuli kwa mwama huu, huko Busan, Korea.
Na ujumbe wa Katibu Mkuu wa WCC,Mchungaji Olav Fykse, kwa ajili yamkutano hua, umeonyesha shukrani kwa ajili ya masuala yaliyozungumzwa wakati wa mjadala. Na kwamba, wako katika maandalizi ya Mkutano huo wa mwaka wa Busan. Na mawazo mengi yaliyo pendekezwa na CCP, yatajadiliwa kwa usahihi zaidi katika Mkutano wa Busan, ambamo kituo cha mkutano, ztakuwa mandhari ya haki, amani na uadilifu katika uumbaji, chini ya kaulimbiu ya amani.










All the contents on this site are copyrighted ©.