2013-03-21 15:02:52

Urafiki na kuheshimiana ni vigezo muhimu kwa watu watamaduni mbalimbali za kidini


Hotuba ya Papa kwa wawakilishi wa Makanisa na Jumuiya za kikanisa na dini zingine.
Jumatano Baba Mtakatifu Francis, alikutana na wawakilishi wa makanisa , jumuiya za Kikristu na dini zingine, ambao walikuwa wamefika Vatican kwa nia ya kushiriki katika Ibada ya Misa, aliyoiongoza, kwa nia ya kuzindua utume wake kama kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki wa 266 tangu kwa Petro Mtume.
Papa Francis, kwa wawakilishi hawa, ilisisitiza umuhimu wa kukuza urafiki na heshima kati ya wanaume na wanawake wa mila za dini mbalimbali. Na alitaka dunia daima kudumisha hamu ya kuwa na imani kwa Ukuu wa Mungu, muumbaji wa vyote vilivyo hai, na kuzikataa tamaa za kutaka kujitukuza na kumdharirisha binadamu kama vile ni kiumbe au bidhaa iliyo tengenezwa na binadamu.

Kabla ya Mkutano huu, Papa kwanza alikukutana na wawakilishi kadhaa binafsi akiwemo Patriaki wa Kiekumene wa Constatinople, Bartholomayo I, na Askofu Mkuu Hilarion, mwenyekiti wa Idara ya Mahusiano ya Nje Kanisa wa Upatriaki wa Moscow.

Papa Francis aliianza hotuba yake kwa kuwashukuru wote waliokuwepo kwa nia yao ya kutaka kumsindikiza wakati akianza utume wake kama Askofu wa Roma, na mrithi wa Petro. Alikiri kuusikia uwepo wa kiroho wa jumuiya wanazo wakilisha na hivyo kupatwa na hisia za kutaka kushiriki hata haraka zaidi katika maombi kwa ajili ya umoja wa waumini wote wa Kristo.
Papa alisema, mabadiliko binafsi katika uhusiano na Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, aliyekufa na kufufuka kwa ajili ya wokovu wetu," ni muhimu kwa kila Mkristo. Na hamu hii ya kutaka kuutangaza ujumbe huu ni kiini cha Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican, , ambao una maana sana hasa katika safari ya kiekumeni.

"Tunaomba Baba mwenye huruma na kutuwezesha kuishi kikamilifu imani kwamba tumepokea kama zawadi katika siku ya Ubatizo wetu, uwezo wa kutoa ushuhuda wetu kwa uhuru, furaha na ushupavu. " Na kwamba kwa kadri tunavyo zidi kuwa aminifu kwa mapenzi yake - katika mawazo, katika maneno na matendo ndivyo tunavyojitahidi kuwa wakweli katika kutembea pamoja kuelekea umoja kamili", Papa Francis aliomba na kusisitiza.

Na akiwageukia wawakilishi kutoka dhehebu la Wayahudi, Papa alizungumzia hasa kiungo maalum cha Kiroho, kati ya Wakristu na Wayahudi. Na alionyesha imani yake kwamba, majadiliano kati ya Kanisa na Wahayudi, yaliyokwisha anzishwa yataendeela na kutoa matunda mema kama ilivyo tazamiwa katika Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican, majadiliano ambayo mpaka yameonyesha mafanikio mengi na matunda mengi, hasa katika kipindi cha miongo kadhaa iliyopita."

Papa Francis , kisha alitaja umuhimu wa mazungumzo kati ya madhehebu, akisema, "Kanisa Katoliki linafahamu na kutambua umuhimu wa kukuza urafiki na heshima kati ya wanaume na wanawake wa mila tofauti za kidini. Kwa ufahamu huo, Kanisa linaona ni wajibu ambao kila mmoja wetu anapaswa kuuzingatia kama dira ya kumwongoza binadamu katika kuvipenda viumbe vyote vya Mungu na kuvilinda.
Aliasa, “tunaweza kufanya mengi kwa ajili ya wale ambao wako katika mazingira magumu , ambao kwa bahati mbaya ni dhaifu au wale wanaoteseka kupitia ukuzaji wa haki na kuimarisha maridhiano na kujenga amani." "Lakini juu ya yote," Papa Francis alihitimisha hotuba yake, ni lazima kuweka hai katika ulimwengu wetu, kiu ya kumtafuta Mungu, na kutoruhusu maono ya binadamu katika mwelekeo wake mmoja kutaka kujitukuza na kutawala, mwelekeo wa mtu kupuuzwa na kuwa kama kitu cha kutengenezwa na binadamu au kama bidhaa nyingine anazozitumia binadamu. Hili ni jambo la hatari zaidi katika nyakati zetu, ameasa Papa Francis.







All the contents on this site are copyrighted ©.