Papa Francis atuma Salaam za Matashi mema kwa Askofu Mkuu Justin Welby
Baba Mtakatifu Francis, Jumatatu iliyopita, alipeleka Salaam za matashi mema kwa Askofu
Mkuu Justin Welby, wa Canterbury, Mkuu wa Jumuiya ya Waanglikani duniani. Katika
salaam hizo, Papa alianza na Maneno: Neema na amani ya Bwana zimiminwe kwako. Na aliendelea
kutoa shukurani zake za dhati kwa Askofu Mkuu Justin, kwa maneno yake mazuri aliyomtumia
mara bada ya kuchaguliwa. Hivyo nae, anapenda kujibu salaam hizo, kwa kumtakia kila
la heri katika utume wake kama Askofu Mkuu wa Kanisa kuu la Canterbury, na Kiongozi
Mkuu wa Wanglikani duniani. Na kwamba utume wa Kichungaji ni wito katika kutembea
kwa uaminifu wa Injili ya Bwana Yesu Kristu. Na amemhakikishia sala zake katika wito
wake huu mpya, ulio dhaminishwa kwake na Bwana wenyewe. Papa anatazamia, wataweza
kukutana muda si mrefu , kwa nia za kuendelea kutia joto katika mahusiano ya kidugu
yaliyofurahiwa na watangulizi wao.