2013-03-21 07:54:17

Mchakato wa Katiba nchini Tanzania unaendelea kwa kasi nzuri, lengo ni kuwa na Katiba Mpya ifikapo mwaka 2015


Waziri mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda katika mahojiano maalum na Radio Vatican anabainisha kwamba, uamuzi wa Serikali ya Tanzania kuanzisha mchakato wa kuandika Katiba Mpya unalenga kuwapatia watanzania Katiba Mpya itakatokuwa ni dira na mwongozo kwa miaka mingine hamsini ijayo. RealAudioMP3

Kwa sasa Tume ya kurekebisha Katiba imemaliza kukusanya maoni kutoka kwa wananchi katika maeneo yote nchini Tanzania. Tume inafanya majumuisho na uchambuzi na hatua inayofuata ni uandikaji wa Rasimu ya Katiba Mpya. Serikali imeanza kuunda Mabaraza ya Katiba kuanzia vijijini hadi Baraza kuu la Taifa, ili kutoa fursa kwa wananchi kurutubisha na kuboresha Rasimu ya Katiba Mpya. Rasimu ikishapitishwa na Baraza kuu la Taifa, itarudishwa tena kwa wananchi ili waweze kuipigia kura ya maoni.

Waziri mkuu Mizengo Pinda akiwa kwenye Studio za Radio Vatican amesema kwamba, hatua ambayo Tanzania imefikia kwa sasa katika mchakato wa kuandika Katiba Mpya inatia matumaini ya kuweza kuwa na Katiba Mpya katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika kunako mwaka 2015.







All the contents on this site are copyrighted ©.