Vijana wako tayari kumpokea Papa Francis wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani,
2013
Askofu mkuu Joao Orani Tempesta wa Jimbo kuu la Rio de Janeiro, Brazil, mwenyeji wa
Maadhimisho ya Siku ya Vijana Kimataifa yatakayoanza kutimia vumbi kuanzia tarehe
23 hadi 28 Julai, 2013 mjini Rio de Janeiro. Waamini na kwa namna ya pekee vijana,
wamepokea taarifa ya kuchaguliwa kwa Kardinali Jorge Mario Bergoglio kuwa Khalifa
wa Mtakatifu Petro kwa mikono miwili. Wanatambua kwamba, kwa hakika wakati wa Maadhimisho
ya Siku ya Vijana Duniani kwa Mwaka 2013 watakuwa na Baba, Mwalimu na Mtumishi wa
watumishi wa Mungu.
Kanisa tayari limekwisha jipanga kumpokea na kumkirimia
Khalifa wa Mtakatifu Petro atakapokwenda nchini Brazil kukutana na kuwaimarisha vijana
katika hija yao ya kujenga na kuimarisha Kanisa, daima wakiwa makini katika kumtolea
ushuhuda Kristo aliyeteswa, akafa na kufufuka kutoka katika wafu!
Askofu mkuu
Tempesta anasema, Kanisa la Amerika ya Kusini, linatambua na kuthamini mchango wa
Baba Mtakatifu Francis wakati wa utume wake alipokuwa nchini Argentina. Kanisa, lakini
vijana kwa namna ya pekee, wako tayari na makini kumpokea Baba Mtakatifu Francis,
wakati wa maadhimisho ya Jubilee ya miaka 25, tangu Siku ya Vijana Duniani ilipoadhimishwa
kwa mara ya kwanza Amerika ya Kusini.