Papa kuanza utume wake rasmi kama Khalifa wa Mtakatifu Petro hapo tarehe 19 Machi
2013
Baba Mtakatifu Francis amemwandikia barua Rabi mkuu wa Roma Riccardo di Segni, akimjulisha
rasmi kwamba, tarehe 19 Machi 2013 ataanza rasmi utume wake kama Khalifa wa Mtakatifu
Petro. Ni matumaini ya Baba Mtakatifu Francis kwamba, atachangia katika kuendeleza
mchakato wa uhusiano mwema kati ya Wayahudi na Wakatoliki, uliotolewa na Mababa wa
Mtaguso mkuu wa Pili wa Vatican; kwa ajili ya kushirikiana katika huduma ili kuleta
mabadiliko duniani, daima wakijitahidi kutekeleza mapenzi ya Mungu.