Makardinali waahidi kushikamana na Baba Mtakatifu katika kulihudumia Kanisa
Kardinali Angelo Sodano, Dekano wa Makardinali kwa niaba ya Makardinali wenzake, wanamshukuru
Mwenyezi Mungu kwa zawadi aliyolijalia Kanisa lake kwa kulipatia mchungaji mkuu mpya.
Wanamshukuru Baba Mtakatifu Francis kwa kukubali kujitwika dhamana ya kuwa ni Khalifa
wa Mtakatifu Petro.
Jambo linalohitajika zaidi ni upendo kwa Kristo katika
kutekeleza dhamana ya kuliongoza Kanisa; dhamana nyeti na inayodai uwajibikaji wa
hali ya juu. Lakini Makardinali wanatambua kwamba, Kristo Mchungaji mwema daima atakuwa
kandoni mwake na ataendelea kumwangazia kwa njia ya Roho Mtakatifu ili aweze kulipyaisha
Kanisa.
Makardinali wamemhakikishia mchango na mshikamano wa dhati wakati anapotekeleza
utume wake katika Kanisa hili linaloendelea kupata mang'amuzi ya Pentekoste mpya,
kila mtu akitenda na kutekeleza dhamana hii mintarafu neema, karama na baraka alizokirimiwa,
ili Mwenyezi Mungu apewe sifa na utukufu.