Maaskofu DRC watuma salam na matashi mema kwa Papa Francis
Familia ya Mungu nchini DRC imepokea kwa furaha na moyo mkuu taarifa za kuchaguliwa
kwa Kardinali Jorge Mario Bergolglio kuwa Khalifa wa Mtakatifu Petro. Katika ujumbe
uliotiwa sahihi na Askofu Nicolas Djomo, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki DRC unasema
kwamba, kuchaguliwa kwa Baba Mtakatifu Francis ni zawadi kutoka kwa Mwenyezi Mungu
kwa ajili ya Kanisa na Dunia kwa ujumla wake.
Baraza la Maaskofu Katoliki DRC
kwa niaba ya Familia ya Mungu nchini humo, linamtakia kheri na baraka Baba Mtakatifu
Francis katika maisha na utume wake kama Khalifa wa Mtakatifu Petro. Bikira Maria
Mama wa Mungu na Kanisa amsindikize katika hija ya utume wake kwa Kanisa la Kiulimwengu.