2013-03-13 08:54:40

Hali ya wananchi wengi wa Kenya baada ya uchaguzi inategemea uwajibikaji makini wa wanasiasa!


Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki-Moon amewapongeza wananchi wa Kenya kwa kushiriki kwa wingi na hatimaye, kufanikisha mchakato mzima wa uchaguzi mkuu uliofanyika hapo tarehe 4 Machi 2013 kwa amani na utulivu na kuyapokea pia matokeo kwa hali ya utulivu, hizi ni dalili za ukomavu wa kidemokrasia na utawala wa sheria.

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa amezungumza kwa njia ya Simu na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta pamoja na Bwana Raila Odinga, aliyewahimiza viongozi hawa wawili kuhakikisha kwamba, wanawatuliza mashabiki wao na kwamba, ikiwa kama kuna mtu akuridhika na matokeo ya uchaguzi badi, akate rufaa kwenye Mahakama kuu, ili haki iweze kupatikana kwa njia ya sheria.

Hali ya wananchi wengi wa Kenya inategemea kwa namna ya pekee uwajibikaji wa viongozi wa kisiasa nchini humo. Kwa mara ya kwanza asilimia 86% ya wananchi wa Kenya waliojiandikisha kupiga kura walishiriki katika zoezi hili la kidemokrasia.







All the contents on this site are copyrighted ©.