2013-03-08 07:56:38

Wanawake ni walezi wa kwanza katika Jamii, changamoto ya kutekeleza wajibu wao!


Bi Imelda Kalolo kutoka Dodoma, Tanzania, katika mahojiano na Radio Vatican anabainisha kwamba, katika ulimwengu wa utandawazi na maendeleo ya sayansi na teknolojia kuna haja kwa wanawake kusimama kidete katika misingi ya imani, maadili na utu wema kwa njia ya mifano bora ya maneno lakini zaidi kwa maisha adili na matakatifu. RealAudioMP3

Wanawake wajitahidi kuwa wachamungu kwa njia ya sala, ili kweli waweze kuwa ni chachu ya utakatifu na maisha adili miongoni mwa vijana wa kizazi kipya, kwa kutambua kwamba, wanawake kimsingi ni walimu wa kwanza wa maisha ya sala na adili kwa watoto wao! Kutokana na mfumo wa maisha kuendelea kubadilika kwa kasi, vijana wengi wanajikuta wanamezwa na malimwengu, kiasi cha kupotoka na kukengeuka!

Hili Jamii iweze kuwa na vijana wenye msingi bora wa maisha adili yanayokubalika mbele ya Mungu na Jamii, kuna haja kwa wanawake kujifunga kibwebwe ili waweze kuwa kweli ni mifano bora ya kuigwa, kwa kutekeleza wajibu wao wa kwanza ambao ni malezi kwa watoto wao! Wazazi wenyewe wawe ni watu wenye msingi bora wa maadili na thabiti katika imani inayojionesha katika matendo. Wasaidie kukoleza miito mitakatifu katika Kanisa kwa kutambua kwamba, Mapadre na Watawa wema na watakatifu wanatokana na Familia bora za Kikristo.







All the contents on this site are copyrighted ©.