2013-03-08 07:53:00

Bado hakuna tarehe ya kikao cha Conclave- Pd Lombardi aeleza


Kikao cha Tano cha Makardinali -bado hakuna tarehe ya kuanza kwa Conclave.
Alhamis, Asubuhi, Makadinali waliendelea na mkutano wao , wakiwa na kikao cha tano, cha kuelekea Mkutano wa Conclave. Na jioni waliketi katika kikao cha sita.
Mkurugenzi wa ofisini ya Habari Vatican, Padre Federico Lombardi, akitoa muhtasari kwa wanahabari: juu ya kikao cha tano, alifahamisha kwamba, bado haijulikani tarehe ya kuanza Conclave. Alitaja idadi ya Makardinali waliohudhuria kikao cha tano kuwa 152. Na kwamba , alikuwa akikosekana Kardinali mmoja tu mwenye haki ya kupiga kura nae ni Kardinali Pham Minh Man, wa Vietnam aliyekuwa akitarajiwa kuwasili Alhamis.
Padre Lombardi, katika mkutano huu, aliwataka wanahabari kusikiliza kinachoelezwa na Ofisi ya habari ya Vatican na kujiepusha na uvumi unaotolewa na wanahabari wasiojua taratibu za mkutano wa Makardinali Consistori na Conclave, kama baadhi ya vyombo vya habari vilivyo ripoti juu ya Ibada za Misa zinazojulikana kwa jina la “Pro eligendo Pontifici ”, wakidhani Ibada hiyo, itakayoadhimisha Jumatatu katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro ndiyo mwanzo wa Conclave. Hiyo si kweli.
Padre Lombardi amefafanua kwamba, Ibada hizo za Pro Eligendo Pontifici zinaweza kuadhimishwa nyingi tu , kwani hutolewa kwa nia za kuombea baraka vikao vya Conclave. Na hivyo, aliendelea, -“Missa Pro eligendo Pontifice” ni Misa inayoweza kuadhimishwa na Padre yeyote, katika siku hizi, kwa nia ya kuomba Roho Mtakatifu alisaidie Kanisa , katika hali hii ya Kiti cha Petro kuwa kitupu. Na hivyo si kila Ibada ya Missa Pro eligendo Pontifici, huwa na nia ya kufungua vikao vya Conclave.
Pia katika kikao cha Alhamis Asubuhi , walichaguliwa wasaidizi wapya wa watatu wa Camerlengo , nao ni Kardinali Boutros Rai Patriaki wa Maronite, akiwakilisha Maaskofu Makardinali , Kardinali Monsengwo kwa Makardinali Mapadre, na Kardinali De Paolis kwa Makardinali Mashemasi, wote watatu watakuwa wasaidizi wa mstari wa Mbele katika dawati la Camerlengo. Kazi watakao ifanya kwa muda wa siku tatu .
Aidha katika kikao hiki cha Tano,katika umoja wao kama Decania ya Makardinali walituma salaam zao za rambirambi , Venezuela , kufuatia kifo cha Rais wa Venezuela Hugo Chavez.
Na pia, waliendelea kusikiliza michango na maoni , kati ya walioshiriki kutoa hoja, kwanza, ni wale wanaohusika na idara za uchumi , Kardinali Versaldi, Calcagno na Bertello. Versaldi ni Gavana wa Mambo ya Uchumi, rais wa APSA, Tawala za urithi wa Kiti cha Kitume, na Bertello ni Rais wa Utawala Vatican.
Na kwamba majadiliano yalifanyika katika utaratibu wa kujali mizania za bajeti, wakianisha ilivyokuwa mwaka uliopita, na matazamio ya mwaka ujao, na kisha kujadiliwa Makardinali 15 na kuchapishwa katika vyombo vya habari hapo Julai , ikifuata utaratibu wake uliopo.
Pamoja na kujadili mengine mada ya uinjiishaji wa Kanisa katika ulimwengu wa leo, Kiti Kitakatifu, idara za Vatican mahusiano na Maaskofu, matarajio na sifa za Kardinali anayefaa kuchaguliwa kuwa Papa, zinaendelea kupewa kipaumbele na muda zaidi katika vikao .








All the contents on this site are copyrighted ©.