Makardinali watuma salam na matashi mema kwa Papa mstaafu Benedikto XVI
Makardinali kwa njia ya simu ya maandishi,, Jumanne tarehe 5 Machi 2013, wamepeleka
salam za matashi mema kwa Papa Mstaafu Benedikto XV1 , ambaye kwa wakati huu anaishi
Castel Gandolfo , Makazi ya Kipapa yaliyoko nje kidogo ya jiji la Roma. Ujumbe huo
unasema: Kwako, Papa Mstaafu Benedikto XV1, Castel Gandolfo. Makardinali
, wakiwa wamekusanyika mjini Vatican kwa ajili ya Mkutano wa kawaida wa maandalizi
ya kikao kijacho cha uchaguzi wa Khalifa wa Mtakatifu Petro, wanapenda kuchukua nafasi
hii kukutimia salaam zao za upendo, kwa mara nyingine wakirudia kutoa shukrani zao
za dhati, kwa mwanga wa fumbo la kiti cha Petro na kwa kuwa kwao, mfano wa Mchungaji
mwema na mnyenyekevu, kwa ajii ya mafao ya Kanisa na dunia kwa ujumla. Shukrani
zao zinalenga kuonyesha utambuzi wa Kanisa zima kwa kazi ulizofanya bila kuchoka
katika Shamba la Bwana. Umoja wa Dekania ya Makardinali , unaendelea kuweka tumaini
katika maombezi yako, kwa ajili yao na kwa ajili ya Kanisa Takatifu. +Kardinali
Andelo Sodano. Dekano wa Dekania ya Makardinali. Kutoka Vatican, 5 Mach 2013.