2013-03-06 07:45:14

Licha ya kasoro ndogo ndogo, wananchi wa Kenya kwa ujumla wameonesha ukomavu wa kidemokrasia!


Askofu Martin Kivuva wa Jimbo Katoliki Machakosi, anawashukuru na kuwapongeza wananchi wa Kenya kutokana na uvumilivu na uzalendo waliouonesha wakati wa mchakato mzima wa uchaguzi mkuu uliofanyika nchini Kenya, hapo tarehe 4 Machi 2013. Kimsingi kumekuwepo na hali ya utulivu licha ya matukio kadhaa ya uvunjifu wa amani yaliyopelekea watu 17 kupoteza maisha yao mjini Mombasa.

Askofu Kivuva anasema, wananchi wengi wamejitokeza kushiriki katika uchaguzi mkuu nchini humo. Makosa katika daftari la wapiga kura ni jambo la kawaida linaloweza kurekebishwa kwa ajili ya mafao ya maendeleo ya wananchi wa Kenya kwa siku za usoni.

Ni matumaini ya Askofu Kivuva kwamba, amani na utulivu vitaendelea kutawala nchini humo ili kujenga na kuimarisha utawala bora unaozingatia mafao ya wengi. Kwa mara ya kwanza wananchi wa Kenya wamepiga kura kwa kutumia Katiba Mpya iliyopitishwa kunako mwaka 2010.







All the contents on this site are copyrighted ©.