Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki-Moon, amewapongeza wananchi wa Kenya
kwa kufanikisha mchakato wa uchaguzi mkuu kwa utulivu na uwazi na kwamba, hii inaweza
kuwa ni hatua makini kwa Kenya katika ujenzi wa demokrasia, amani na utulivu.
Umoja
wa Afrika umeonesha kuridhishwa kwake na hali ya uchaguzi nchini Kenya, uliofanyika
katika "hali ya amani na utulivu". Viongozi wanasikitishwa na idadi kubwa ya kura
zinazohofiwa kwamba, zimeharibika. Serikali ya Marekani inawataka wananchi wa Kenya
kuhakikisha kwamba, malalamiko yote kuhusu uchaguzi yanapatiwa ufumbuzi kwa njia ya
sheria, ili kutolitumbukiza tena taifa kwenye maafa kama ilivyojitokeza katika chaguzi
kadhaa zilizopita.