Siku ile Yesu akatoka nyumbani, akaketi kando ya bahari. Wakamkusanyikia makutano
mengi, hata akapanda chomboni, akaketi; nau le mkutano wote wakasimama Pwani. Yesu
alifundisha kwa mifano mingi: juu ya Mpanzi na kuwafafanulia maana ya mifano hii kadiri
ya mchakato wa ujenzi wa Ufalme wa Mungu.
Anasema, Manabii wengi na wenye
haki walitamani kuyaona mnayoyaona, lakini wasiyaone; na kuyasikia mnayosikia lakini
wasiyasikie! Yesu akafafanua kwa kina kuhusu Magugu, Punje ya haradali, Chachu na
kwamba, hayo yote Yesu aliwaambia makutano kwa mifano, wala pasipo mfano hakuwaambia
neno, ili litimie neno lililonenwa na Nabii, akisema ”nitafumbua kinywa changu kwa
mifano, nitayatamka yaliyositirika tangu awali.
Katika mifano yote hii Yesu
anakazia umuhimu wa kutubu na kuongoka kwa kujivika fadhila ya unyenyekevu kama watoto
wadogo. Anazungumzia kuhusu makwazo na kuwaonya wote wanaowakwaza wengine kwamba,
kwa hakika watakiona cha mtema kuni! Anawaalika kuonyana kidugu, kusali pamoja na
kusameheana wao kwa wao wakitambua kwamba, Bwana yu kati yao!
Yesu anawaonya
wafuasi wake dhidi ya chachu ya Mafarisayo, bali ushuhuda wao ujioneshe katika maneno
na matendo. Yesu pia alichukua fursa ile kukemea mji wa Yerusalem ambao pia unasifika
kwa kutenda mauaji ya Manabii waliotumwa kutangaza Habari Njema ya Wokovu. Yesu anawataka
wafuasi wake wasidanganyike na Manabii wa uwongo, dhuluma na taabu mbali mbali watakazokutana
nazo.
Lakini atakayevumilia hadi mwisho, huyo ndiye atakayeokoka. Tena habari
Njema ya Wokovu itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote;
hapo ndipo ule mwisho utakapokuja! Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu anasema
Yesu hayatapita kamwe! Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata
Malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.