Roma yaanza kusali kwa ajili ya mchakato wa kumpata Papa Mpya!
Kardinali Agostino Vallini, Makamu Askofu Jimbo kuu la Roma, kwa niaba ya Waamini
wa Jimbo la Roma, anapenda kumshukuru Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, ambaye
ameng'atuka rasmi kutoka madarakani kwa kumhakikishia kwamba, wataendelea kusali kwa
ajili yake na Kanisa, wakati huu Makardinali wanapoanza mchakato wa uchaguzi wa Papa
Mpya, ili kuendeleza dhamana na utume wa Khalifa wa Mtakatifu Petro.
Kardinali
Vallini anawaalika viongozi wa Kanisa kutumia fursa hii pia kutoa Katekesi ya kina
kuhusu Ukulu na Dhamana ya Mtakatifu Petro katika kuliongoza Kanisa la Kristo, pamoja
na kusali kwa ajili ya kumpata Papa Mpya. Anaendelea kuwaalika Watawa wa Mashirika
ya ndani kusali zaidi kwa ajili ya mchakato wa kumpata Khalifa Mpya wa Mtakatifu Petro.