Makardinali kuanza mchakato wa kumtafuta Papa Mpya hapo tarehe 4 Machi 2013
Kardinali Angelo Sodano Dekano wa Makardinali katika taarifa yake kwa vyombo vya habari
anasema kwamba, mkutano wa kwanza wa Makardinali watakaoshiriki katika mchakato wa
kumchagua Papa Mpya utaanza rasmi, Jumatatu, tarehe 4 Machi 2013, saa 3:30 katika
Ukumbi wa Sinodi ya Maaskofu. Kuna uwezekano pia wa kufanyika mkutano wa pili baadaye
jioni.